• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhimira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Uchumi Mipango na Takwimu
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo
      • Elimu ya Sekondari
      • Afya
      • Maji Vijijini na Taka Ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
    • Huduma za Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Ratiba ya vikao vya wah.Madiwani
      • Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
      • Muongozo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mikakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu
      • Fomu za Maombi
    • Miongozo
    • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kata ya Lugelele

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBARALI

KATA YA LUGELELE


Mhe. Nelson P. Vicent

DIWANI WA KATA

 

NEEMA SALO

AFISA MTENDAJI WA KATA

+255 765 518 341

 

TAARIFA YA KATA

1. UTANGULIZI 

Kata ya Lugelele ni kati ya kata 20 zilizopo katika Wilaya ya Mbarali Tarafa ya Rujewa, na umbali wa kilometa 7 kutoka makao makuu ya Wilaya na Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali. Kata ya Lugelele ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa

Kata ya Lugelele ndipo yalipo makao makuu ya Wilaya ya Mbarali pamoja, Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali na ipo ndani ya Mji Mdogo wa Rujewa, vilevile Kata hii imepakana na kata za Rujewa, Mapogoro na Wilaya ya Wanging’ombe Mkoa wa Njombe. 

Katika ngazi ya Kata kuna Viongozi ambao ni Diwani wa Kata na Afisa Mtendaji wa Kata na kwa upande wa Vitongoji kuna Wenyeviti wa Vitongoji 38.

Kata ya Lugelele ina jumla ya watumishi 97 wa kada mbalimbali kama ifuatavyo: Utawala 1, Elimu watumishi 86, Afya watumishi 3, Maliasili watumishi 0, Kilimo watumishi 4, Mifugo 2 na Maendeleo ya jamii watumishi 1. 

Kata ya Lugelele ina jumla ya wakazi wapatao 8,673 kati yao Wanaume 4,262 na Wanawake 4,411. Makabila yanayopatikana katika Kata ya Lugelele ni Wasangu, Wabena, Wagogo, Wasukuma, Wamasai na Wahehe. 

Shughuli kubwa za kiuchumi kwa wananchi wa kata hii ni Kilimo, Mifugo na Biashara. 

Vyanzo vya Mapato katika kata hii inatofautiana kutokana na Kijiji kimoja hadi kingine, miongoni mwa vyanzo hivyo ni kama; faini/adhabu mbalimbali, pawatila, michango ya wananchi, Ruzuku kutoka Serikali kuu (Halmashauri ya Wilaya) pamoja na misaada kutoka kwa Wadau mbalimbali. 

Vivutio vya utalii vinavyopatikana katika kata ni pamoja na Misitu ya asili na pori la akiba la Mpanga Kipengere eneo la Igomelo

Hali ya Ulinzi na Usalama ndani ya kata ni nzuri kabisa kwani hakuna matukio ya kuhatarisha usalama. Aidha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya kata inafanya kazi ikiwemo kushirikiana na vitongoji kufanya doria usiku na mchana vilevile kuna kituo cha polisi Wilaya kilichopo kata ya jirani ya Rujewa umbali wa Km 11 ambapo sambamba na majukumu mengine huhakikisha ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao.

2. HUDUMA ZA KIJAMII ZINAZOTOLEWA PAMOJA NA FURSA ZILIZOPO 

 A. ELIMU 

Kata ya Lugelele ina Jumla walimu wa Serikali 86, shule za Msingi za Serikali 4, shule ya sekondari binafsi 1, Na shule ya sekondari ya Serikali 1.

 i. ELIMU MSINGI 

Shule za Serikali 

  • Shule ya Msingi Igomelo
  • Shule ya Msingi Mlomboji
  • Shule ya Msingi Kanioga
  • Shule ya Msingi Mayota 

 ii. ELIMU SEKONDARI

Shule za Serikali 

  • Shule ya Sekondari Igomelo,

Shule za Binafsi 

  • Shule ya Sekondari Mbarali River Side

B. AFYA 

Kata ya Lugelele ina watumishi wa idara ya afya 3, na zahanati 1 ambayo ni Zahanati ya Igomero,Vilevile kuna Hospital ya Wilaya ambayo ipo kata ya jirani ya Rujewa umbali wa km 11 kutoka makao makuu ya kata. Magonjwa yanayosumbua mara kwa mara ni ; Diarrhea, URTI upper respiratory Infection, Pneumonia, UTI- Unary track Infection, fracture –(Dislocation), Surgical condition, Burn, Skin Infection Fungal, Skin Infection non fungal na Fungal Infection non skin.

C. KILIMO, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

Kata ya Lugelele ina jumla ya watumishi 4 idara ya kilimo na ushirika, na ina jumla ya wakulima 1,281, wanawake 474 wanaume 1,281. Mazao yanayopatikana katika kata ya ni Mpunga, Mahindi, Alizeti, Mtama, Viazi Vitamu, Maharage, Karanga, Nyanya na Vitunguu

idadi ya skimu za umwagiliaji zilizopo ni Igomelo, Kanioga na Mayota. Vilevile kuna chama cha ushirika kimoja ambacho Chama cha Ushirika na Umwagiliaji Igomelo

Huduma zinazotolewa na Wataalam wa Kilimo ni ;

  • Huduma za ugani
  • Mashamba darasa juu ya Kilimo cha Kisasa
  • Hifadhi bora ya Mazao ya Chakula
  • Elimu juu ya ushirika
  • Ukaguzi wa vyama vya ushirika pamoja na ushauri wa namna ya kuviendesha na kuvisimamia
  • Kutatua Migogoro ya Wakulima na Wafugaji
  • Elimu ya masoko na stakabadhi ghalani
  • Ushauri juu ya matumizi sahihi ya maji
  • Ushauri juu ya matumizi sahihi ya zana za Kilimo na pembejeo
  • Ushauri juu ya Kilimo bora cha Mazao
  • Kukusanya takweimu za Mvua
  • Kuandaa na kutoa taarifa ya Utekelezaji ya kila robo mwaka na kuwasilisha wilayani.
  • Kuandaa na kutoa taarifa ya Utekelezaji wa Maendeleo ya Kilimo katika Kamati ya Maendeleo ya kata.

D. MIFUGO NA UVUVI

Kata ya Lugelele ina jumla ya watumishi 2 wa idara ya mifugo na Uvuvi na ina Jumla ya Mifugo kama ifuatavyo:

  • NG’OMBE         3860
  • MBUZI              3661
  • KONDOO          818
  • MBWA              796
  • NGURUWE       238
  • PUNDA             151

Magonjwa yanayosumbua mifugo mara kwa mara ni kama, Babesiosis,PPR, New Castle na Ndui

Huduma zinazotolewa na Idara ni pamoja na;

  • Tiba kwa magonjwa dhidi ya Mifugo
  • Huduma mbalimbali za Mifugo kama kuhasi, kukata pembe, kwato na midomo, kupiga chapa Mifugo, kukata meno, kuzalisha, kuogesha na Ukaguzi wa nyama
  • Ushauri juu ya ujenzi bora wa mabanda ya Mifugo
  • Kutoa elimu ya ufugaji bora wa namna ya ufugaji wa Mifugo yenye tija
  • Ukaguzi wa Nyama na usafi katika Machinjio
  • Kusimamia zoezi Endelevu la upigaji chapa wa mifugo

Sekta ya Uvuvi ni mojawapo ya sekta zinazofanya kazi katika kata hii. Idara inaendelea kushauri wananchi juu ya uchimbaji bora wa mabwaya ya samaki kwa ajili ya ufugaji wenye tija.

E. MALIASILI

Kata ya Lugelele haina watumishi wa maliasili mpaka sasa, na Kata ya Lugelele ina uhifadhi wa misitu.

 i.Vivutio vya Utalii                                        

  • Misitu ya asili na
  • pori la akiba la Mpanga Kipengere eneo la Igomelo

 ii. Hifadhi ya Misitu

Kata ya Lugelele inaendelea kuhamasisha wananchi juu ya ulinzi na utunzai wa hifadhi kwa kushirikiana na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS), kupanda miti, kuzuia uharibifu wa mazingira kwa kuchoma mkaa na kukata miti hovyo bila ya kuipanda upya, pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya uoteshaji na upandaji miti.

 ii. Mikakati ya uhifadhi wa mazingira pamoja na faida inayopatikana kutokana na uhifadhi huo. 

Kata inaendelea kutoa hamasa kwa wananchi pamoja na taasisi kuhusiana na kuendelea kulinda mazingira hasa maeneo ya misituasili na vyanzo vya maji kwa matumizi endelevu, kuendelea kushauri kutengwa kwa bajeti kwa ajili ya uoteshaji na upandaji wa miti katika Vitongoji.


F. MAENDELEO YA JAMII

Kata ya Lugelele ina mtumishi mmoja wa Idara ya Maendeleo ya Jamii mpaka sasa, huduma zinazotolewa na kata ni kama ifuatavyo;

  • Uandikishaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka 5
  • Elimu ya ulinzi na usalama wa mtoto
  • Elimu ya kupinga ukatili kwa akina mama na watoto
  • Kutetea haki za wazee, watoto na jamii kwa ujumla
  • Kuhamasisha wananchi kujiunga na bima ya afya
  • Kuhamasisha wazazi kupeleka watoto shuleni
  • Kufuatilia shughuli za kiuchumi zinazofanywa na wanufaika wa Tasaf
  • Kufuatilia Utekelezaji wa Kamati za ukimwi vijijni (VMAC)
  • Kuhamasisha Wanawake, Vijana na Walemavu juu ya shughuli mbalimbali za ujasiliamali
  • Kuhamasisha shughuli za Maendeleo kwenye mikutano na vikundi
  • Kusimamia shughuli mbalimbali za Maendeleo vijijini.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA KAZI YA MKATABA YA MTUNZA KUMBUKUMBU (DATA ENTRY CLERK) NA TABIBU (CLINICAL OFFICER II) TAREHE 02-12-2022 November 28, 2022
  • RE-ADVATISEMENT JOB VACANCIES November 10, 2022
  • MPANGO MKAKATI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBARALI 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • Tazama

Taarifa Mpya

  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI AKISHIRIKI ZOEZI LA USAFI KATIKA KATA YA UBARUKU

    March 03, 2023
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI KANALI DENIS MWILA AKISHIRIKI ZOEZI LA USAFI NA UPANDAJI WA MITI WILAYA YA MBARALI TAREHE 18/02/2023

    February 24, 2023
  • TIMU YA CMT MBARALI NA MENEJA WA MAJI WILAYA YA MBARALI WAKIKAGUA MRADI WA MAJI

    May 15, 2022
  • AFISA UTUMISHI NA UTAWALA

    June 09, 2022
  • Tazama

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Tovuti Mashuhuri

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

Ramani kwa wasafiri

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Sanduku la Posta: 237 Rujewa Mbeya

    Simu ya Mezani: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Barua Pepe: ded@mbaralidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.