• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Primary Education

KAZI ZA IDARA

Idara ya Elimu Msingi ndiyo yenye dhamana na kusimamia na kuratibu shughuli zote zinazohusu elimu Msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali. Shughuli hizo ni kama ifuatavyo:- 

  • Kuratibu shughuli zote zinazohusu taaluma katika Halmashauri
  • Kusimamia utendaji kazi wa walimu na watumishi wa idara ya Elimu na wasio kuwa walimu.
  • Kuratibu takwimu zote za Idara ya Elimu kama vile Miundombinu, vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, n.k, idadi ya wanafunzi, walimu na nyinginezo.
  • Kuratibu Maslahi ya walimu kama likizo, madai mbalimbali kama vile uhamisho, mizigo na malimbikizo ya mishahara pamoja na kupanda madaraja.
  • Ulinzi na usimamizi wa mali za Umma zitumikazo katika Uendeshaji wa Elimu msingi kama vile Samani za shule, maeneo ya shule na mali nyingine.
  • Kudhibiti utoro wa walimu na wanafunzi na kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria, taratibu na Kanuni za Elimu na nchi kwa ujumla

 

HUDUMA ZINAZOTOLEWA KATIKA IDARA YA ELIMU MSINGI 

Idara ya Elimu Msingi inatoa huduma mbalimbali zinazohusiana na mambo ya Elimu na Taaluma kwa wanafunzi, wananchi na Walimu kwa ujumla. Vilevile Idara hii hutoa huduma kama inavyoelekezwa na Mkurugenzi wa Halmashauri wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali kwa kuzingatia miongozo, nyaraka na maelekezo mbalimbali. Baadhi ya Huduma zitolewazo ni kama ifuatavyo:

  • Kushughulikia uhamisho wa wanafunzi na walimu
  • Kushughulikia likizo za walimu na watumishi na wasio walimu wanaohudumia katika Idara ya Elimu msingi
  • Kushughulikia masuala ya kinidhamu na utoro wa walimu na wanafunzi.
  • Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wazazi, wanafunzi na walimu kwa ujumla
  • Maslahi ya walimu kama madaraja n.k
  • Huduma mbalimbali zinazohusiana na taaluma

VITENGO VILIVYOPO IDARA YA ELIMU SEKONDARI

TAALUMA

  • Kusimamia ufundishaji na ufungaji shuleni.
  • Kufanya usajili wa wanafunzi wanaofanya mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) na upimaji wa kitaifa wa Darasa la nne (SFNA).
  • Kwa kushirikiana na Afisa Elimu Watu Wazima kusimamia vituo na madarasa ya elimu nje ya mfumo rasmi na elimu masafa.
  • Kufanya tathimini ya matokeo ya mitihani yote ya kujipima Wilaya, Mkoa na mitihani ya kitaifa.
  • Kupitia taarifa za ukaguzi wa shule zinazofanywa na Idara ya Uthibiti Ubora wa Shule na kuyafanyia kazi mapendekezo waliyoishauri Idara ya Elimu Msingi.

ELIMU MAALUM

  • Kutoa ushauri wa kitaaluma kuhusu huduma ya watu wenye ulemavu.
  • Kufuatilia na utoaji wa Elimu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.
  • Kusimamia ukusanyaji na utunzaji wa Takwimu za wanafunzi wenye ulemavu.
  • Kufuatilia uandikishaji wa watoto wenye mahitaji maalum.
  • Kufuatilia upatikanaji wa vifaa saidizi vya wanafunzi na vifaa vya kufundishia na kujifunzia vya wanafunzi wenye mahitaji maalum.

ELIMU WATU WAZIMA

  • Kumshauri Afisa Elimu Msingi kuhusu masuala ya Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya mfumo rasmi EWW/ENMRA.
  • Kusimamia utekelezaji wa sera ya Elimu watu wazima Elimu nje ya mfumo rasmi EWW/ENMRA.
  • Kubaini mipango ya kuendeleza taaluma ya Elimu Watu Wazima na Elimu nje ya mfumo rasmi.
  • Kuratibu mashindano ya kitaaluma ya Elimu watu wazima Elimu nje ya mfumo rasmi EWW/ENMRA katika Halmashauri.
  • Kukusanya, kuchanganua na kutayarisha taarifa za utekelezaji wa Elimu watu wazima Elimu nje ya mfumo rasmi EWW/ENMRA wa kutoa taarifa.

ELIMU TAKWIMU NA VIFAA (SLO)

  • Upanuzi na uimarishaji wa Elimu Msingi.
  • Kusimamia na kufuatilia ujenzi wa shule.
  • Ukusanyaji, uhifadhi na utoaji wa takwimu za Elimu Msingi (kuzipokea, kuzichanganua, kuzifafanua na kuziwasilisha zinakotakiwa bila kuchelewa).
  • Mahitaji ya walimu – kufanya makisio ya idadi kwa daraja kufuatana na upungufu na upanuzi.
  • Vifaa vya shule – uagizaji na usambazaji kufuatana na mahitaji ya shule na fungu la fedha.
  • Mtihani – usimamizi, usafirishaji na usalama wake
  • Kusimamia fedha katika Idara matumizi yalingane na mahitaji.
  • Kufanya kazi zingine mtakazopewa na Afisa Elimu Wilaya.

UTAMADUNI NA MICHEZO

  • Kuandaa na kuratibu shughuli za michezo ya wanafunzi wa shule za msingi (UMITASHUMTA) shule za Sekondari (UMISSETA) na watumishi walio chini ya mamlaka ya Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA).
  • Kuratibu shuhguli za Mwenge wa Uhuru.
  • Kukagua kumbi zinazojishughulisha na upigaji disko pamoja na sherehe mbalimbali (burudani mbalimbali).
  • Kuandaa mabonanza ya michezo kwa wanafunzi na watumishi wa Taasisi mbalimbali za Umma na za watu binafs.
  • Kutoa vibali vya matangazo mbalimbali ya biashara na yasiyo ya kibiashara, mikutano, burudani za aina zote.
  • Kutoa mafunzo ya sanaa za maonesho, ufundi na lugha pamoja na kuandaa matamasha ya utamaduni.
  • Kutoa ushauri kwa Mkuu wa Idara juu ya mashuala ya utamaduni na michazo.

 

MATARAJIO YA IDARA 

Idara inatarajiwa kufanya mambo yafuatayo:

  • Kupandisha kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi wanaofanya mitihani ya Taifa kama vile Mitihani ya Darasa la Nne na la Saba
  • Kuamsha ari ya utendaji kazi kwa walimu ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi.
  • Kujenga uhusiano mzuri baina ya walimu, wanafunzi na Jamii inayozunguka shule (wananchi)
  • Kuhakikisha maslahi ya walimu yanaboreshwa na kupatikana kwa wakati kama vile fedha za likizo, uhamisho, kupanda madaraja kwa walimu, makazi bora ya walimu, upatikanaji wa vifaa vya kusomea na kufundisha kwa wakati.
  • Kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa Elimu na kuwapatia watoto elimu bora.
  • Kuendesha vikao vya wadau wa Elimu katika Halmashauri ili kuleta tija katika elimu





Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.