• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

DC Akataa Siasa Katika Utekelezaji wa Mambo ya Maendeleo.

Posted on: November 6th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe. Reuben Mfune, amewataka viongozi wote katika Wilaya ya Mbarali kuacha masuala ya kisiasa katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwenye wilaya yake kwani mambo hayo ya kisiasa wawaachie watu wanaohutubia kwenye majukwaani wakati wa kampeni za kuomba kura, yeye anachotaka ni kuona miradi ya maendeleo inatekelezwa.

Mhe. Mfune ameyasema hayo alipokuwa kwenye mwendelezo wa ziara zake katika kata za Igava, Miyombweni pamoja na Madibira siku ya tarehe 05/11/2018 kwa ajili ya kufuatilia maagizo aliyoyatoa kwa viongozi wa kata na vijiji  kuhusiana na ujenzi wa vyumba vya madarasa, Ujenzi wa zahanati, ujenzi wa vyoo, masuala ya lishe pamoja na uandikishaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5.

Kuhusiana na ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja na zahanati, Mkuu wa Wilaya ameipongeza Kata ya Igava kwa kutekeleza maagizo aliyoyatoa kwa asilimia kubwa kwani wamekamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja na kufikia hatua nzuri kwenye ujenzi wa zahanati kwa kila kijiji, ila amewataka zoezi hilo la ujenzi wa madarasa liende sambamba na utengenezaji wa madawati.

“Naridhika na Kata ya Igava katika utekelezaji wa maagizo ya Serikali, mnafanya vizuri katika ujenzi wa zahanati na madarasa endeleeni na spidi mliyonayo, tukikamilisha wote tutaunganisha nguvu katika ujenzi wa kituo cha afya”

Katika hatua nyingine, Mhe. Mfune amezipongeza Kata za Miyombeni na Madibira kwenye suala la uhamasishaji kwa wananchi kujenga vyoo, kwani kwa hatua walizofikia, ni kaya chache tu katika kata hizo ambazo hazijakamilisha ujenzi vyoo ukilingazisha na Kata ya Igava ambapo kuna kaya zipatazo 576 ambazo hazina vyoo kabisa.

“Kaya 576 kukosa vyoo ni tatizo kubwa, wote tunajua kwanini tunahamasisha watu kuhusu  ujenzi wa vyoo.  Lazima watu wajenge kwa vyoo kwa nguvu, hatuwezi kubembelezana suala linalogusa afya zetu, kila mtu lazima awe na choo, kilo 10 za simenti (saruji) zinaweza kutengeneza  choo kikasafishika na ukiweka sinki la plastiki aina ya SATTO unapata choo bora. Tuendelee kuhamasisha wananchi”

Aliongeza kuwa kufikia tarehe 01/12/2018 hataki kusikia kuna kaya ambayo haina choo katika Wilaya yake ya Mbarali sababu kwa sasa tunakoelekea kipindi cha masika, na safari hii hataki kusikia tena magonjwa ya milipuko kama kipindupindu na kuhara maana wote ni mashahidi kwa kilichotokea mwaka 2017 watu zaidi ya 800 waliugua ugonjwa kipindupindu na baadhi walipoteza maisha na moja ya sababu kubwa iliyopelekea ugonjwa huo ni kukosa vyoo kwa baadhi ya kaya.

Kuhusiana na Uandikishiji wa Vyeti vya Kuzaliwa pamoja na Masuala ya Lishe, Mhe. Mfune alisema kuwa, mambo haya ni endelevu, ni vyema tukatumia sehemu zetu za kuabudia katika kutoa elimu ya vitu hivi.

“Tutenge walau dk 10 kwa ajli ya kutoa elimu ya lishe na kupata vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5, tuwaelekeze wananchi umuhimu wake Katika kila mkutano wa hadhara wa kijiji kwa kuwa masuala haya ni endelevu.  Kwa sasa vyeti vya kuzaliwa vinatolewa bure kwa wototo wenye umri wa chini ya miaka 5, baada ya hapo watalazimika kuvilipia.  Wenyeviti wa vijiji pamoja na watendaji tengenezeni utaratibu na muwatangazie wananchi mzunguko wa uandikishaji wa vyeti vya kuzaliwa na katika shughuli zenu za kawaida muwe mnapita kwenye kaya zenu na kuuliza kama kuna watoto ambao hawajaandikishwa.”

“Siku 1000 ndio kipindi cha kujenga  ubongo wa mtoto, na hizo siku zinaanzia tangu mimba inapotungwa hadi mtoto anapotimiza miaka 2, na baada ya hapo haitawezekana tena kumrekebisha,  tunakusudia kutunga sheria ndogo ili wale watakaokaidi kuwapeleka watoto wao kupata utambuzi wa lishe wachukuliwe hatua, lengo letu ni kuepuka kuwa na kaya zenye watoto wenye udumavu au lishe duni. Tunataka kujenga taifa la kesho lililoelimika vizuri kupambana na changamoto na kupiga hatua katika maendeleo”

Mkuu wa Wilaya amemaliza ziara katika kata zote 20 kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kujenga vyumba vya madarasa, kujenga zahanati kwa kila kijiji, kujenga vyoo, uandikishaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5 pamoja na masuala ya lishe tangu inapotungwa mimba hadi mtoto anapofukisha umri wa miaka miwili (siku 1,000).

Mkuu wa Wilaya anatarajia kufanya mkutano na waandishi wa habari siku ya alhamisi ya tarehe 08/11/2018 na kutoa maelekezo ya ujumla kuhusiana na ziara alizozifanya.

MWISHO

Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.