• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

“Kuna Utaratibu wa Kufuata Kuwaondoa Viongozi wa Vijiji”

Posted on: November 18th, 2017

Hayo yamesemwa  na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe Reuben Mfune kwenye mkutano wa hadhara aliouitisha kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za Wananchi wa Kijiji cha Ijumbi kilichopo Kata ya Ruiwa Wilaya ya Mbarali siku ya tarehe 17/11/2017.

Akiongea na wananchi wa Kijiji hicho katika mkutano huo, Mhe mfune alisema kuwa, alipokwenda katika Kijiji hicho mwezi uliopita aliwaambia kuwa jukumu la kumuondoa Mwenyekiti na Wajumbe ni la wananchi waliomchagua, na angeagiza Halmashauri ambayo inasimamia Vijiji waendelee na mchakato kama mwenyekiti hatoshi kwa mujibu wa tuhuma zake aondolewe kwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa Sheria, wataalamu walishakuja na utaratibu umetumika kwa ajili ya kumuondoa mwenyekiti, vilevile  kama Mwenyekiti hajaridhika na maamuzi ya kumuondoa anaweza kwenda kukata rufaa kwa Mkuu wa Mkoa.

“Sikuja hapa kuja kuwalinda watu waliochaguliwa kama hawafai kuendeleza Kijiji, kama hawawezi kupeleka maendeleo yetu mbele,wapo kwa maslahi yao na tuna uhakika na ushaidi basi utaratibu ufuatwe kuwaondoa”

Kuhusu suala la kusoma mapato na matumizi ya Kijiji, Mhe Mfune ameagiza ndani ya siku saba uitishwe mkutano mkuu wa Kijiji kwa ajili ya kuwasomea wananchi mapato na matumizi ya Serikali yao, vilevile ameagiza kila baada ya miezi mitatu wananchi wasomewe mapato na matumizi ya Serikali yao.

Mhe. Mfune amewaasa Serikari ya Kijiji kutojichukulia madaraka ya kufanya kila kitu bila ya kupata ridhaa ya wananchi kupitia mikutano mikuu ya Kijiji, vitu vyote vinavyoletwa kwa ajili ya maslahi ya wananchi kutoka sehemu mbalimbali, mfano mabati, simenti na mengineyo  lazima kuwaeleza wananchi, Serikali ya Kijiji inatakiwa kupendekeza matumizi ya bidhaa hizo na kuwasilishwa kwa wananchi kwa ajili ya kupitisha matumizi yake.

Kuhusu suala la mifugo maeneo ya misitu katika Vijiji vya Motomoto na Malamba, Mhe Mkuu wa Wilaya alishapiga marufuku kwa wale wanaolima, wanaojenga na wanaochunga mifugo yao kwenye maeneo hayo au kwenda kufanya shughuli za kibinadamu kwani kufanya hivyo  kunaharibu eneo la hifadhi ya misitu ambayo ni vyanzo vikubwa vya maji katka maeneo Wilaya yetu, na kuna watu wanaohusika na amewaweka kwa ajili ya kulinda eneo hilo la hifadhi ya misitu, kwa maeneo ambayo watu wanakata miti na wanachoma mkaa hasa kata ya Ipwani, kuna  baadhi ya watu wameshawakamatwa na wapo polisi na magari yao na watachukliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

 Akizungumza katika mkutano huo, Afisa Utumishi na Utawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, Ndg. Aswege Kaminyoge, alitoa utaratibu wa kuwaondoa viongozi wa Serikali za Vijiji ambapo alieleza kuwa, Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa, Majiji pamoja na Vijiji zimeanzishwa na sheria namba 7 ya mwaka 1982, ni utaratibu wa kisheria kwa Serikari ya Kijiji kufanya shughuri za kila siku za uendeshaji wa Kijiji.

“kwa mujibu wa sheria kwa Vijiji vilivyosajiliwa vinatakiwa kukutana kila baada ya miezi mitatu ambayo ni mara nne kwa mwaka, mwenyekiti wa Serikari ya kijiji pamoja na Mtendaji wa Kijiji kwa kushirikiana na wajumbe wa Serikali ya kijiji wana wajibu wa kuitisha mikutano hiyo”

Kaminyoge aliongeza kuwa, suala la kumuondoa Mwenyekiti madarakani pamoja na wajumbe wa Serikali, kwa  mujibu wa taratibu na kanuni zilizotungwa mwaka 1995, wenye mamlaka ya kumuondoa Mwenyekiti ni Halmashauri ya Serikali ya Kijiji yenye watu 25 kwa kupiga kura mara baada kupitia tuhuma zilizopatikana kwenye mikutano mikuu ya Vijiji kwa wananchi ambao walimchagua.

Kwa upande wa Wajumbe wa Serikali za Vijiji, alisema kuwa, wenye mamlaka ya kuwaondoa madarakani ni mkutano mkuu wa Kijiji, kama mjumbe ana tuhuma au ana mwenendo mbaya katika Serikali, kitakachofanika ni kwamba, itatolewa hoja ya kutokuwa na imani na mjumbe huyo, anaweza akawa mmoja au wawili au zaidi waliotuhumiwa, itajadiliwa kwenye mkutano huo, baada ya hapo itapigwa kura ya kutokuwa na imani nae au nao, ili kuweza kuwaondoa wanatakiwa kufuata utaratibu huo.

Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.