• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Mkutano Mkuu wa Kijiji ndio wenye Mamlaka ya Kugawa Ardhi ya Kijiji-Kyando

Posted on: March 7th, 2020

Hayo yamesemwa na mjumbe wa Kamati Maalumu ya Uelimishaji Wananchi Juu ya Umuhimu wa Uhifadhi na Ujirani Mwema, Afisa Mipango Miji Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndg. Enock Kyando alipokuwa akiwasilisha mada yake ya matumizi bora ya Ardhi katika vijiji vya Uturo, Mtamba, Ukwama na Kapunga Wilaya ya Mbarali siku ya tarehe 07/03/2020.

Kyando alisema kuwa wanakijiji wanapaswa kuzisimamia Serikali zao za kijiji ili ardhi yao isichukuliwe bila kufuata utaratibu kwani kuna baadhi ya sehemu baadhi ya viongozi wamekuwa sio waaminifu wanagawa ardhi ya kijiji bila kuwashirikisha wenye ardhi yao.

*“Msimamizi mkuu wa ardhi ya Kijiji ni Serikali ya kijiji kupitia mkutano mkuu, mtu yeyote anaehitaji kumiliki ardhi ya kijiji anatakiwa kupitishwa kwenye mkutano mkuu ili apangiwe matumizi ya ardhi aliyoiomba, Mtendaji na Mwenyekiti kazi yao ni kupokea maombi tu, Ardhi ni kitu cha muhimu, tusipoisimamia vizuri tutakuja kupigana wenyewe kwa wenyewe”* alisema Kyando

Kyando aliongeza kuwa kijiji kinatakiwa kuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi kwani itaondoa migogoro ya mipaka mbalimbali vilevile ni chombo kinachoonesha ni kiasi gani cha ardhi kilichopo kwa ajili ya shughuli za kijiji kama mifugo, kilimo, makazi, viwanda pamoja na matumizi mengine.

Aliongeza kuwa sambamba na kuwa na matumizi bora ya ardhi ya kijiji ni vizuri kila mtu mwenye kipande cha ardhi akachukua hati yake ya kimila yake ambayo inapatikana ofisi ya kijiji ili awe amemiliki kisheria kwani Hati miliki ya kimila ina hadhi sawa na hati miliki zingine za ardhi.

Aidha, Mjumbe mwingine wa timu ya uelimishaji Afisa Mipango Miji Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Ndg Geofrey Mwaijobele amesema kuwa ardhi haiongezeki bali wanadamu na mifugo ndio vinaongezeka kwa kasi hivyo ni muhimu Serikali za vijiji kuweka kipaumbele mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kuepusha migogoro ya wakulima na wafugaji.

Mwaijobele ameongeza kuwa kama maeneo ya misitu na malisho ya mifugo yamehifadhiwa na kijiji ni vyema kila mwananchi akahusika kuyalinda maeneo hayo.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria kwenye mikutano hiyo wameishukuru timu ya uelimishaji iliyoundwa kwani wameongeza uelewa wa masuala ya uhifadhi, kwani walikuwa wanavunja sheria bila kujiua na kupitia elimu hiyo watawaelimisha na wengine ili kudumisha ujirani mwema na wahifadhi.

Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.