• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

TASAF SASA KUTUMIA MFUMO WA KIELECTRONIC KULIPA KAYA MASIKINI

Posted on: July 10th, 2020

Hayo yamesemwa na Meneja Miradi ambaye ni Kiongozi wa Timu ya Taifa kwa ajili ya kazi ya Uhakiki wa kaya kutoka TASAF Makao Makuu Ndg Shabani Abdumalick alipokuwa akiendesha kikao kazi kwa Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na mafunzo ya kuwajengea uwezo wawezeshaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali kuhusu utekelezaji wa kipindi cha pili awamu ya tatu ya Tasaf  na  zoezi la uhakiki wa walengwa wa kaya masikini siku ya terehe 09/07/2020.

Ndg. Shabani alisema kuwa malipo yote kwa sasa yanatarajiwa kulipwa kwa kutumia mfumo wa Kielectronic kwa wanufaika watakuwa wanapokea malipo yao kwa kutumia simu zao, kwa njia ya mawakala au dawati la Bank kwa lengo la kupunguza gharama za usafiri pamoja na changamoto zilizojitokeza katika awamu iliyopita.

 

“Zoezi la sasa linatarajiwa kufanyika kwa njia ya mfumo wa kielectronic, na baadae tutaacha kutumia magari kupeleka pesa vijijini, mlengwa atatakiwa kuleta namba ya simu iliyosajiliwa na kwa ambao hawatakuwa na simu tutawawekea utarabu unaofaa. Tunanza uhakiki kwa kutumia vishikwambi (Tablet) ambazo zitakuwa zikitumika kubeba dodoso fupi litakalofanya kazi ya uhakiki wa taarifa.

 

“kinachofanyika kwa sasa ni uhakiki ili kusafisha daftari libaki na kaya ambazo zina sifa za kuendelea kuwa kaya masikini ili ziweze kuendelea kupata rudhuku ya Serikali kutoka TASAF. Tunahakiki kaya zote zilizo kwenye mpango wa TASAF kwa nchi nzima na katika zoezi hili hakutaongeza kaya mpya, kaya ambazo hazitafika kufanyiwa uhakiki, hazitalipwa” Alisema Ndg Shabani

Akisoma taarifa wakati wa ufunguzi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Taifa Ndg. Ladislaus Mwamanga, Bwana. Shabani alisema kuwa utekelezaji wa kipindi cha kwanza cha TASAF awamu ya tatu umechangia kwa kiasi kikubwa azma ya Serikali kupunguza umaskini nchini kwani mahitaji ya msingi kwa Kaya yamepungua kwa asilimia 10 na umasikini uliokithiri umepungua kwa asilimia 12.

Aliongeza kuwa baada ya kukamilisha kipindi cha kwanza cha awamu ya tatu ya TASAF Serikali iliamua kuendelea  na kipindi cha pili ili kaya zote zinazoishi katika mazingira duni zipate usaidizi kwa kuwawezesha kufanya kazi na kupambana na umasikini.

 

“Kipindi hiki kitazifikia ya kaya 1,450,000 zenye jumla ya watu zaidi ya milioni 7 kote nchini ikiwa ni nyongeza ya kaya zaidi ya 350,000. Kutakuwa na miradi mbalimbali inayotekelezwa ikiwemo miradi ya Elimu, Afya na Maji”

 

“Itatengenezwa miradi ambayo itawalazimu walengwa waweze kufanya kazi ili waweze kupata kipato. Miradi hiyo itakuwa inatoa ajira za muda lengo likiwa mtu apate sababu ya kulipwa kwa kufanya kazi” alisema kwa Niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Tasaf

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Ndg. Aswege Kaminyoge, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuanzisha Tasaf awamu ya 3 kwani itaziwezesha kaya nyingi kufanya kazi kwenye miradi itakayoibuliwa na kuweza kujipatia kipato, na kwa niaba ya Halmashauri wapo tayari kutekeleza miaradi yote itakayoletwa kwa asilimia 100.

Akiongezea mratibu wa Tasaf Wilaya ya Mbarali Ndg. Zabron Abel alisema kuwa, kwa kupitia mafunzo yaliyotolewa kwa mfumo wa kielectronic kwa wawezeshaji ngazi ya Wilaya wanatarajia watapita katika vijiji 75 vilivyopo kwenye mpango kuzihakiki kaya 10,317 kwa lengo la kuwa na data safi za walengwa, na ili waweze kuhakikiwa watalazimika kuja na kitambulisho cha Mpango, daftali la mototo kwa wale ambao wanasoma, namba ya simu, pamoja na namba ya Nida au kitambulisho cha mpiga kura.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wawezeshaji kwa njia ya mfumo kwenye mafunzo hayo, Bi. Helen Ngowo na Bwana. Edwin Mgendwa wameishukuru Serikali kwa kuleta TASAF awamu ya 3 sehemu 2 kwani awamu hii inatumia zaidi mfumo kwa kutumia Vishikwambi (Tablet) ambazo zitawasaidia kupata kaya zenye sifa zitakazostahili kuwepo kwenye mpango na itawezesha kuondoa walengwa hewa.

MWISHO

Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.