• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

DC Awakemea Wanaosuasua Kuanza Ujenzi wa Zahanati

Posted on: October 31st, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe. Reuben Mfune, amevitaka vijiji vyote ambavyo havijaanza ujenzi wa Zahanati katika Wilaya ya Mbarali kuanza mara moja ndani ya mwezi wa 11.

Mhe. Mfune ameyasema hayo alipokuwa kwenye mwendelezo wa ziara zake katika kata za Mawindi na Ipwani zilizopo tarafa ya Rujewa siku ya tarehe 30/10/2018 kwa ajili ya kufuatilia maagizo aliyoyatoa kwa viongozi wa kata na vijiji  kuhusiana na ujenzi wa vyumba vya madarasa, Ujenzi wa zahanati, ujenzi wa vyoo, masuala ya lishe pamoja na uandikishaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5.

“Nataka ndani ya mwezi wa 11, zahanati zote wilayani mbarali ambazo hazijaanza kujengwa, ziwe zimeanza kujengwa”

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya amewapongeza viongozi wote wa kata ya Ipwani wakiongozwa na Diwani wa Kata hiyo Mhe. Marcusi Kalinga kwa hatua nzuri waliyofikia katika kukamilisha ujenzi wa shule ya sekondari Ipwani kwani kukamilika kwake kutasaidia  upatikanani wa elimu kwa wanafunzi wa kata ya Ipwani.

“Nimevutiwa na hatua ya Ujenzi mliyofikia, hadi sasa kuna mabadiliko makubwa tangu nilivyofika awamu iliyopita mwezi julai, wananchi wamejitahidi sana nipo tayari tuitishe harambee ili kumalizia vitu vilivyobaki, kwani kukamilika kwa shule hii kutapunguza mzigo katika shule jirani ya Mawindi”

Vilevile Mhe. Mfune ameendelea kuwasititiza wananchi wote kujenga vyoo bora ili ifikapo tarehe 01/12/2018 suala la kutokuwa na vyoo liwe historia katika wilaya ya Mbarali na amewaagiza viongozi wote kuanzia ngazi ya kata hadi vijiji kuwafikisha kwenye mabaraza ya kata wale wate ambao hawana vyoo mpaka sasa.

“Kuna baadhi ya watu wanajua kula tu, ila kujenga vyoo hadi tulazimishane, majadilianao ya kujenga vyoo yafikie mwisho, tunataka kufikiria kujenga zahanati, vyumba vya madarasa pamoja na mambo mengine ya maendeleo, vilevile adhabu itolewe kwa wale waliojenga  vyoo ila hawavitumii”

“Niwapongeze Kata ya Ipwani kwa kufanyia kazi suala la kutokuwa na vyoo, sasa tuhame kutoka kwenye vyoo vya asili kwenda kwenye vyoo bora, choo bora ni choo kilichojengwa kwa tofari, kinachosafishika, kilichoezekwa na kuwa na mlango, hatufanyi haya ili kujifurahisha ila ni kuepukana na magonjwa ya mlipuko”

Kuhusiana na Masuala ya lishe na uandikishaji wa watoto wenye umri chini ya miaka mitano na kupata vyeti vya kuzaliwa, Mhe. Mfune alisema kwamba mambo haya ni endelevu, yanahitaji kutolewa elimu kila mara, viongozi wa vijiji na kata wanatakiwa kutoa japo dakika 10 kwa waelimishiji kwenye kila mikutano hadhara ili elimu hii ziweze kutolewa.

“Vyeti vya kuzaliwa vina faida nyingi sana, sasa hivi mtoto ni lazima awe na cheti cha kuzaliwa, vyeti hivi chini ya miaka 5 vinatolewa bure, baada ya hapo watatakiwa kuvilipia, tuendelee kuhamasisha ili kila mtoto aweze kuandikishwa.”

“Mtoto akikua na hali ya udumavu kila kitu kinavia, sababu ubongo unakuwa haujakua vizuri, tuendelee kuelimisha wananchi madhara na faida zake na ifike mahali ambapo mtu ambaye hampeleki mtoto wake kupimwa utambuzi wa hali ya lishe (ukondefu, uzito pungufu na udumavu) apigwe faini na faini hizo zitumike kusidia kuwajengea vyoo wale ambao hawajiwezi.”

MWISHO

Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.