• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Madiwani Kyela Wafanya Ziara ya Mafunzo Mbarali

Posted on: November 29th, 2017

Waheshimiwa Madiwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kyela wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo  Mhe. Hunter A. Mwakifuna pamoja na baadhi ya Wataalamu wamefanya ziara ya kujifunza namna ya matumizi ya bora ya “Force Account” na namna bora ya kuzuia vifo vya mama na mtoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali siku ya tarehe 28/11/2017.

Akiwakaribisha wageni hao Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Mhe. Francis Mtega, alishukuru ujio wa wageni hao na kuwatajia fursa mbalimbali zinazopatikana Wilayani hapa, ikiwemo kilimo cha mpunga ambacho kinatumia maji kidogo na ndio chanzo kikubwa cha mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali.

Katika ziara hiyo wameweza kujifunza matumizi ya “Force Account (utekelezaji wa kazi kwa kutumia mafundi wa kawaida bila ya kutumia wakandarasi)” kutoka shule ya Sekondari Rujewa ambapo, Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiaa na Wizara ya Elimu Sayansi na Technolojia kupitia Program ya Lipa Kulingana na Matokeo (P4R) ilitoa fedha za ujenzi na ukarabati kupitia akaunti ya shule ya Sekondari Rujewa kiasi cha Tsh. 259,000,000.00/=. Fedha hizo zilitakiwa zitumike katika Ujenzi wa Miundombinu, kama Ujenzi wa Mabweni Mawili (2) kwa ajili ya kidato cha tano na sita pamoja na vitanda,mabweni hayo yana uwezo wa kuchukua wanafunzi 80 kwa kila moja kwa gharama ya Tsh. 150,000,000.00, Ujenzi wa vyumba vinne (4) vya madarasa vyenye meza na kiti kwa thamani ya Tsh. 80,000,000.00/=, Umaliziaji/ukarabati wa maabara kwa thamani ya Tsh.18,000,000.00 pamoja na Ujenzi wa matundu kumi ya vyoo kwa thamani ya Tsh.11,000,000.00

Wakiwa katika zahanati ya Uturo ambayo ndio zahanati ya mfano kitaifa katika kudhibiti vifo vya mama na mtoto, zahanati hiyo kwa muda wa miaka 19, Tangu mwaka 1998 hakuna vifo vya watoto wachanga wala wazazi vinavyotokana na matatizo ya uzazi vilivyotokea katika kijiji cha Uturo. Wakiwa katika zahanati hiyo iliyopo Wilaya ya Mbarali kata ya Mapogoro kijiji cha Uturo wameweza kujifunza mambo mablimbali ambayo yatasaidia kupunguza na kukomesha vifo dhidi ya mama na mtoto.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Mhe Hunter A. Mwakifuna amemshukuru Mganga mfawidhi ndugu Wilson Chotamganga na Wananchi wa Kijiji cha Uturo kwa juhudi zao na kuweza kufanikisha jambo hilo.

“Wananchi wameelewa kuwa zahanati hii ni mali yao, na wametusubiri tangu asubuhi, namshukuru Mganga mfawidhi ndugu Wilson Chotamganga na namtakia kila la kheri katika likizo yake ya kustaafu” alisema Mhe. Mwakifuna

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Ndg Mussa J. Mgata amepongeza ubunifu uliofanyika katika zahanati hiyo na kuahidi kuwachukua baadhi ya wataalamu na akinamama waliounda kikundi cha kupambana na vifo vya mama na mtoto kwenda Wilayani Kyela kutoa mafunzo.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Mhe. Broun Kwakibete amewashukuru kwa kufanya ziara ya kuja kujifunza mambo kuhusu matumizi ya "Force Account" na namna ya Kuzuia Vifo vya Mama na Mtoto, na ameahidi kuwa nao watakwenda kujifunza mambo mbalimbali katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela.

Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.