• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Mhe. Rais Magufuli awataka wananchi wa Mbarali wasubiri uamuzi wa Serikali juu ya hatma ya Vijiji 33 vilivyopo ndani ya Hifadhi

Posted on: May 3rd, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli amewataka wakazi wa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya kuendelea kuvuta subira wakati wakisubiri uamuzi wa Serikali juu ya hatma ya vijiji 33 ambavyo kutokana na Tangazo la Serikali namba 28 la mwaka 2008 (GN namba 28) inavitaja kuwepo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

Mhe.Rais Magufuli aliyasema hayo siku ya tarehe 02/05/2019 alipohutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Barafu uliopo katika Kata ya Rujewa wilayani Mbarali.

Alisema kuwa, ripoti ya Tume ya Mawaziri nane iliyoundwa ilikwisha kamilisha kazi yake na kukabidhi taarifa kitakachofuata ni kumalizia mgogoro huo.

Amewataka wakazi wa Mbarali kuondoa hofu kwani atahakikisha maamuzi yatakayofanyika yanabeba maslahi mapana ya wananchi wa Mbarali hasa ikizingatiwa kuwa wana uhitaji mkubwa wa ardhi kwaajili ya shughuli za kilimo na ufugaji

 “nataka niwaambie ndugu zangu wa Mbarali, Serikali mliyoiweka madarakani kamwe haiwezi kuwaonea, naomba mtuamini tufanyie kazi ripoti ya Mawaziri na tutaleta majibu, lakini kile kijiji cha machimbo ambacho wananchi wake walidai fidia na walilipwa takribani shilingi Milioni 800, hao itabidi waondoke” 

Aidha Mhe. Rais amewaagiza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Willium Lukuvi, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Albert Chalamila, Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe. Reuben Mfune na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya ya Mbarali Ndg. Kivuma Msangi, kumpelekea orodha ya wananchi waliogawiwa ekali 6027 kutoka kwa wawekezaji waliogawiwa mashamba ya Mpunga ya Kapunga na Highland Estate.

Pamoja na kuagiza apatiwe orodha hiyo Mhe. Rais Magufuli amempongeza mwekezaji wa shamba la Highland Estate ambae ni Mbunge wa Jimbo la Mbarali Mhe. Haroon Mulla Pirmohmed kwa kuachia sehemu ya shamba na kutoa Matrekta madogo 102 (Power Tillers) kwa vijiji vyote vya Jimbo la Mbarali na amewaonya watu wanoafanya udalali wa kuwakodisha wakulima mashamba  kwa gharama kubwa ikilinganishwa na kiwango kilichowekwa na wawekezaji hao.

Vilevile amewaonya wananchi wa Wilaya ya Mbarali kuacha majungu dhidi ya viongozi wao akiwemo Mhe. Mbunge na amewasihi kushikamana na kujielekeza kuijenga Wilaya yao ya Mbarali kwani  majungu wanayoyafanya kwa viongozi wao yanawachelewesha kufanya maendeleo.

Kwa upande wake Mhe. Waziri Lukuvi alisema ripoti ya tume ya Mawaziri nane iliyokuwa maalumu kwaajili ya kupitia maeneo yenye mgogoro wa ardhi kati ya vijiji na hifadhi za Taifa nchini ilikwisha kabidhiwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi ikiwa na mapendekezo yaliyozingatia maoni ya wananchi wakiwemo wa Mbarali.

Mhe. Lukuvi alisema ripoti hiyo imebeba kwa asilimia kubwa ukweli wa unafuu kwa wakazi wa wilayani hapa hivyo muhimu kwao ni kuvuta subira.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mbarali, Mhe. Mhe. Haroon Mulla Pirmohmed aliishukuru Serikali kwa jitihada inazofanya katika kushughulikia suala la GN namba 28 akisema ni jambo linaloleta faraja kwa wananchi wanyonge.

Mwisho.

Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.