• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Mkuu wa Wilaya Awataka Wananchi Kupanda Mikorosho ili Kujiongezea Kipato

Posted on: February 8th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mh. Reuben Mfune amewataka wananchi wa Wilayani Mbarali kupanda miche ya zao la Korosho kwenye mashamba makubwa pamoja na majumbani ili kujiongezea kipato pamoja na kuboresha afya.

Ameyasema hayo siku ya uzinduzi wa upandaji wa miche ya zao la Korosho Kiwilaya liliyofanyika katika Kata ya Mawindi Kijiji cha Manienga siku ya jumanne ya tarehe 06/02/2018

Mh. Mfune alisema kuwa, Watafiti kutoka kituo cha Utafiti wa Kilimo Naliendele waliona hali ya hewa ya Wilaya ya Mbarali inafaa kwa upandaji wa zao la Korosho na waliahidi kushirikiana na wananchi wa Wilaya ya Mbarali kuanzisha kilimo cha zao la hilo na kuleta vilaba pamoja na vifaa kwa ajili ya kuotesha miche 21,000 na hadi sasa Wilaya imefanikiwa kuotesha miche ya Korosho 17,000 ambayo ni sawa na asilimia 81.

“Katika Wilaya yetu kila mtu anafikilia sehemu ambazo maji yanaingia kwa ajili ya kuotesha mpunga, katika maeneo ambayo hatuwezi kuotesha mpunga ndio sehemu sahihi ambayo tunaweza kuotesha korosho, kwa mwaka huu tunategemea kuotesha miche kwenye hekta 240. Nawasihi wananchi wa Wilaya ya Mbarali, tusitegemee zao la punga peke yake, tuwe za zao la biashara la mpunga lakini pia tuwe na zao korosho,” alisema

Mh. Mkuu wa Wilaya aliongeza kuwa Kilimo cha Korosho kina faida nyingi zikiwemo, kutupatia Korosho ambazo kwa sasa kilo moja inauzwa tsh. 4,000, inatunza vizuri moyo, ina madini ambayo yanaimarisha mifupa, kupunguza uzito, inatupatia matunda aina ya mabibo ambayo yanaweza kuliwa kawaida au kutengenezea kinywaji aina ya mvinyo au wine, kuongeza kipato, kutupatia mti wa kivuli, na ni rahisi kuutunza.

Naye Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Ndg. Dickson Kamwela kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji aliongeza kuwa, Wilaya ya Mbarali katika msimu wa kilimo 2017/2018 imekusudia kuanzisha kilimo cha zao la korosho ili kuboresha maisha ya wananchi kwa lengo la kujiongezea kipato. Kilimo cha korosho kinaendeshwa kwa kushirikiana na Kituo cha Utafiti wa Kilimo Naliendele Mtwara na Bodi ya korosho Tanzania.

“Katika msimu huu wa kilimo, Wilaya kwa kushirikiana na watafiti wa kilimo Naliendele na Bodi ya korosho imeanzisha vitalu vya korosho katika kata za Madibira, Rujewa, Mapogoro na Chimala vyenye jumla ya miche 17,019, vitalu hivyo vinasimamiwa na kutunzwa na vikundi/taasisi na watu binafsi.” Alisema

Baadhi Wananchi wa Kata ya Mawindi waliohudhuria uzinduzi huo, walimpongeza Mh. Mkuu wa Wilaya na Wataalam wake kwa jitihada walizozichukua kuhakikisha kilimo cha Korosho kinafanikiwa wilayani Mbarali, kwani kuna sehemu nyingi wilayani hapa zao la mpunga halikubali, ujio wa zao la korosho litakuwa mkombozi mkubwa kwao kwani litaongeza kipato cha mtu mmoja mmoja.

Zao la Korosho linachukua miaka minne kukua na kuvuna mvuno wa kwanza. Tafiti zinaonyesha kuwa mvuno wa kwana unatoa kilo 0.5 na utakapotimiza miaka 10 unaweza kutoa kilo 25 kwa mti mmoja.

Ekali moja ya zao la korosho linaweza kupandwa miche 69 ambayo kwa muda wa miaka 10 inauwezo wa kuzaa kilo 1,725 ambayo kwa bei ya sasa ya sokoni inaweza kumuingiza mkulima kiasi cha tsh 6,900,000.

Zao la korosho halizuii kupanda Mazao mengine madogo magodo kama mikunde, mahindi na karanga kipindi mti unaendelea kukua

Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MAKABIDHIANO YA OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBARALI

    July 03, 2025
  • DED MPYA AWASILI MBARALI

    June 30, 2025
  • KIKAO CHA MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBARALI NA WATUMISHI WOTE WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBARALI

    June 16, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MBARALI YAPATA HATI SAFI BAADA YA UKAGUZI WA CAG

    June 17, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.