• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI

Posted on: February 11th, 2021

TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI 

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, limepitia na kupitisha mapendekezo ya mpango wa Bajeti kiasi cha Sh. 45,890,254,767.49 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kutoka vyanzo mbalimbali vya Mapato siku ya tarehe 11/02/2021.

Kati ya fedha hizo, Mapato kutoka Serikali Kuu na Wadau wa Maendeleo ni Sh. 40,990,998,767.49 na Mapato kutoka katika vyanzo vya ndani (Own Source) Sh. 4,899,256,000.00. Mgawanyo wa fedha hizo ni kama ifuatavyo Sh. 31,036,186,000.00 ni Mishahara, Sh. 5,176,754,785.49 ni Matumizi ya kawaida na Sh. 9,677,313,982.00 ni Miradi ya Maendeleo.

Mpango na Bajeti ya Miaka Mitatu 2021/22- 2023/24 na Makisio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka 2021/22 umeandaliwa kwa kuzingatia, Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala (CCM) 2020-2025, Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndg. John Pombe Joseph Magufuli wakati wa kufungua rasmi Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dodoma Tarehe 13 Novemba, 2020.

Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti Serikali kwa mwaka 2021/22 uliotolewa na Wizara ya Fedha na Mipango, Vipaumbele vya Serikali ya awamu ya tano, Maagizo ya Viongozi wa Kitaifa, Mpango Mkakati wa Halmashauri wa Mwaka 2018/19 - 2023/24, Mpango Mkakati wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR- TAMISEMI),

Mpango Mkakati wa Lishe wa Taifa, Sheria ya Bajeti Na. 11 ya mwaka 2015 na Kanuni zake, Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025, Mpango wa Maendeleo Endelevu 2030, Mapitio ya Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka 2020/21, pamoja na Vipaumbele vya wananchi wa Wilaya ya Mbarali kupitia Mfumo ulioboreshwa wa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (Improved Opportunities and Obstacles to Development- O&OD)

Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali inafikia malengo ya kuwahudumia wananchi wake kupitia Mpango wa Miaka Mitatu 2021/22- 2023/24, Sekta za Kilimo, Mifugo, Elimu Msingi, Elimu Sekondari, Ardhi na Maendeleo ya Jamii zitaonesha matokeo chanya ya malengo katika kutekeleza mpango wa miaka mitatu

Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali katika bajeti yake ya mwaka 2021/22 itajikita katika kuendelea na Ujenzi Miradi ya Kimkakati iliyopata fedha kutoka Serikali kuu ambayo ni Kituo cha Afya Utengule Usangu na Hospitali ya Wilaya, Kuwezesha ukamilishaji wa ujenzi wa banio katika Skimu ya Umwagiliaji Ukwavila, Kuwezesha ujenzi wa vivusha maji vitatu (3) katika Skimu ya Umwagiliaji Msesule, Kuwezesha usakafiaji wa mfereji mita 40 skimu ya umwagiliaji Azimio Mswiswi (FAO).

Kuendelea na ujenzi wa kituo cha Afya Mahongole, kuwezesha uchimbaji wa visima katika Shule za Sekondari za Ihanga- Mbarali na Ipwani, Kujenga shule ya Msingi ya Mchepuo wa Kiingereza (English Medium Primary School), Kuwezesha wakulima 70 kuzalisha mbengu za kuazimia ubora (QDS) tani 210 katika Kongani 3 za Rujewa, Madibira na Igurusi.

Kuendelea na ujenzi wa Shule ya Wasichana Uturo, Kuendeleza ujenzi wa miundombinu katika Shule za Sekondari na Msingi, Kutoa usaidizi katika Jitihada mbalimbali za wananchi katika Vijiji na Kata, Kuboresha miundombinu katika Sekta ya Kilimo na Mifugo, Kuboresha Lishe kwa watoto, Ulipaji wa madeni mbalimbali, Kuwezesha vikundi vya wanawake, vijana na walemavu.

Kuendelea kupambana na Maambukizi ya VVU/UKIMWI, Kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika Uchumi wa Viwanda, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia ya Nchi (Climate Change) pamoja na kutambua jitihada za Jamii katika Kukabiliana na Mabadiliko hayo pamoja na Kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri kwa kuboresha vyanzo vya mapato vilivyopo pamoja na kubuni vyanzo vipya.

Katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2020/21, Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali iliidhinishiwa matumizi ya jumla ya Sh. 45,930,332,615.00  kati ya hizo Sh. 32,090,368,000.00 ni matumizi ya mishahara, Sh. 3,937,500,000.00 ni Mapato ya ndani, Sh. 1,159,244,999.00. ni matumizi mengineyo NHIF Sh. 300,000,000.00, CHF Sh. 100,000,000.00, User Fee Sh. 150,000,000, Ada za Wanafunzi Sh. 40,250,000.00, Michango ya Jamii (EK, Minara, nk) Sh. 144,256,000.00 na Sh. 8,008,713,616.00 ni matumizi ya miradi ya maendeleo.

Hadi kufikia Disemba, 2020, Jumla ya Sh. 18,596,749,460.65 zilipokelewa kati ya hizo, Sh. 13,939,100,697.00 ni fedha za mishahara, Sh. 718,750,500.00 ni fedha za matumizi mengineyo, Sh. 1,650,395,929.81 ni miradi ya maendeleo na Sh. 2,120,112,010.95 ni makusanyo ya ndani, NHIF Sh. 28,109,060.00, CHF Sh. 48,281,266.29 na User Fee Sh 48,399,496.60 na ada za wanafunzi Sh. 43,600,500.00.00. Hii ni sawa na asilimia 40.49 ya fedha zilizoidhinishwa kwa mwaka 2020/2021.

Kwa taarifa zaidi tembelea http://mbaralidc.go.tz/announcement/muhtasali-wa-bajeti-ya-halmashauri-ya-wilaya-ya-mbarali-ya-mwaka-2021-2022


Daudi B. Nyingo

Afisa Habari

Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali

11/02/2021

Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.