• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbarali District Council

  • Home
  • About Us
    • Our History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administrations
    • Organization Structure
    • Departments
      • Finance
      • Administration Natural Resources
      • Works and Fire
      • Primary Education
      • Economy Planning and Statistics
      • Land and Natural Resource
      • Agriculture
      • Secondary Education
      • Hearth
      • Rural Water and Sanitation
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Environmental and Solid Waste
    • Units/Sections
      • Procurement and Surprises
      • ICT Units
      • Law
      • Internal Auditor
      • Bee
      • Election
  • Investment
    • Tourism
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
      • Primary Education
      • Secondary Education
    • Water Services
    • Agriculture
    • Livestock and Fisheries
    • Staff Services
  • Councilors
    • Councilors List
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Permanent Committee
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Councelors Time Table
      • District Chair Personal Time Table
  • Projects
    • Planned Projects
    • Completed Projects
    • Ongoing Project
  • Publications
    • By Laws
      • Guidlines
    • Costumer Services Contract
    • Strategies
    • Reports
    • Forms
      • Application Form
    • Guidelines
    • Publications
  • Media Centre
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

VIJIJI 102 KUWAKA UMEME IFIKAPO AGOSTI 2019 MBARALI

Posted on: April 22nd, 2018

Waziri wa Nishati Mhe. Medard Kalemani amevihakikishia vijiji vyote 102 vilivyopo Wilaya ya Mbarali kufikiwa na huduma ya umeme ifikapo august 2019.

Mhe. Waziri ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kata ya Igurusi siku ya jumamosi ya tarehe 21/04/2018 alipofanya ziara wilayani hapa kwa ajili ya kuzungumza na wananchi pamoja na kuzindua Upanuzi wa Huduma za Umeme Vijijini.

“haya yote ni maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. John Pombe Magufuli katika kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi” alisema.

Akizunguzmza katika ziara hiyo Mhe. Kalemani alisema kuwa, Wilaya ya Mbarali ina Jumla ya vijiji 102, kati ya vijiji hivyo, vijiji 68 vimeunganishiwa umeme mwaka 2017 na vikaongezwa vingine 18 kufikisha Jumla ya vijiji 86 kwenye mradi wa Rea Awamu ya Pili. Kwa vijiji 16 vilivyobaki vitapatiwa umeme kwenye mradi unaotekelezwa kwa sasa Rea Awamu ya Tatu ambapo tayari Mkandarasi yupo kazini.

Vilevile Mhe. Waziri ametoa muda wa siku 10 kwa wananchi 330 ambao hawakuunganishiwa umeme katika mradi wa Rea Awamu ya Pili kuunganishwa mara moja vinginevyo Mhe. Mkuu wa Wilaya awachukulie hatua wote watakaokwamisha agizo hilo.

“Serikali imegharamia huu mradi kwa asilimia 100, mwananchi atalazimika kuchangia kiasi cha shilingi 27,000 tu, isitokee mtu akawalaghai mkatoa pesa zaidi ya hiyo, na kama kuna mwananchi ana nyumba ya nyasi, hiyo ndio ninataka ianze sasa” alisema.

Meneja wa TANESCO Wilaya ya Mbarali Ramadhani Mwanga katika taarifa yake alieleza kuwa, Mradi wa Rea Awamu ya Pili ambao umetekelezwa na Mkandarasi M/s JV State Grid Electronical ulihusisha ujenzi wa njia kubwa ya msongo wa KV33 yenye urefu wa Km 357.29 pamoja na msongo mdogo wa 0.4KV yenye urefu wa Km 144.29 ikihusisha na usimikwaji wa Mashine Umba (Transfomer) 89 na jumla ya wateja 6,449 kwa vijiji 68 wameunganishiwa katika awamu hii na mkandarasi anaendelea kuwaunganishia wateja 330 waliobaki.

Kwa mradi wa Rea Awamu ya Tatu unaotekelezwa na Mkandarasi Steg International Services, Mwanga alisema kuwa jumla ya vijiji 18 vimeshafikiwa na umeme kwani upimaji na usanifu umekamilika na wamefanikiwa kuwatambua wateja 1,507 ambao wapo ndani ya mita 30 na kwa sasa zoezi la kuunganisha umeme linaendelea na hadi kufikia tarehe 31/03/2018 wateja 472 wameunganishiwa kati yao 9 ni wa viwanda vidogo vidogo.

Aliongeza kuwa kwa Mradi wa Rea Awamu ya Tatu itaongeza vijiji 16 vilivyobaki kukamilisha idadi ya vijiji 102 vilivyopo Wilaya ya Mbarali kunufuika na huduma ya umeme na tayari Mkandarasi ameshaanza kusimamisha nguzo katika mtaa wa Mlimani ulipo katika kata ya Rujewa karibu na eneo la mnadani.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe. Reuben Mfune aliongeza kuwa asilimia 83 ya wananchi wa Mbarali wanategemea Kilimo, umeme kwa Mbarali ni muhimu sana kuchochea Maendeleo kwani mara baada ya Kilimo Mazao yote yanachakatwa kwa njia ya umeme, vilevile amemshukuru Mhe. Waziri kwa Kufanya ziara katika Wilaya ya Mbarali kwani amejibu kero zote zinazowatatiza wananchi wa Mbarali.

Diwani wa Kata ya Igurusi Mhe. Hawa Kiwhele akizungumza kwa niaba ya wananchi, amemshukuru Mhe. Waziri kwa ujio wake, kwani ametatua kero kubwa ya umeme inayowasumbua wananchi wake wa Kata ya Igurusi na Wilaya ya Mbarali kwa ujumla.



Announcements

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MBARALI DC- STRATEGIC PLAN WORD 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIZINDUA NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MBARALI MHE KANALI MAULID HASSAN SURUMBU AKIPANDA MTI WAKATI WA KUTEMBELEA MRADI WA KUSINDIKA MAZIWA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA UNAOTEKELEZWA NA KIKUNDI CHA NOPADEO WOMEN GROUP CHA KATA YA ITAMBOLEO KIJIJI CHA MATEBETE

    June 06, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA DKT JUMA ZUBERI HOMERA AKIPANDA MTI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NYEREGETE

    June 05, 2025
  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • View All

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
More Videos

Quick Links

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Related Links

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Postal Address: 237 Rujewa Mbeya

    Telephone: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Email: ded@mbaralidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.