• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mbarali District Council
Mbarali District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhimira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Fedha
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Uchumi Mipango na Takwimu
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo
      • Elimu ya Sekondari
      • Afya
      • Maji Vijijini na Taka Ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
    • Huduma za Maji
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
      • Kata ya Mahongole
      • Kata ya Ruiwa
      • Kata ya Imalilosongwe
      • Kata ya Igurusi
      • Kata ya Itamboleo
      • Kata ya Mwatenga
      • Kata ya Kongolo Mswisi
      • Kata ya Mawindi
      • Kata ya Luhanga
      • kata ya Madibira
      • Kata ya Utengule Usangu
      • Kata ya Igava
      • Kata ya Rujewa
      • Kata ya Mapogoro
      • Kata ya Ipwani
      • Kata ya Miyombweni
      • Kata ya Ubaruku
      • Kata ya Lugelele
      • Kata ya Chimala
      • Kata ya Ihahi
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Time Tabe
      • Ratiba ya vikao vya wah.Madiwani
      • Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
      • Muongozo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mikakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu
      • Fomu za Maombi
    • Miongozo
    • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

PESCODE VICOBA YATOA MEZA NA VITI 52 MBARALI

Tarehe ya Kuanza: February 26th, 2021

Shirika lisilokuwa la Kiserikali linalojihusisha na utoaji wa elimu  ya uanzishwaji wa vikundi vya kijamii vinavyojishughulisha na uwekaji wa akiba, kukopesha sambamba na kutoa elimu ya usimamizi, ujasiliamali, mafunzo ya uongozi pamoja na uandaaji wa taarifa (PESCODE VICOBA) kwa kushirikiana na vikundi vya VICOBA  Mbarali wametoa msaada wa Viti na Meza 52 vyenye thamani ya kiasi cha shilingi 2,080,000 kwa shule ya sekondari ya Igomero siku ya tarehe 26/02/2021.

Akipokea Viti hivyo pamoja na Meza Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe. Reuben Mfune amelishukuru shirika hilo la PESCODE VICOBA pamoja na vikundi vya VICOBA vilivyoshilikiana kutengeneza madawati hayo kwani kufanya hivyo kunaonesha nia ya kusaidia ukuaji wa elimu wilayani hapa.

 

“Kwanza  nawashukuru kwa kupata wazo la kutengeneza madawati, hili wazo limetokana na nyie wenyewe, hamjashinikizwa na mtu yeyote lakini mkaona kuna umuhimu wa kusaidia wanafunzi. Kupitia madawati haya vijana wetu 52 watakaa na kufanya shughuli zao za kusoma vizuri bila tatizo lolote.”

 

“Kuna taasisi nyingi zenye uwezo hazijaweza kufanya kama mlivyofanya nyie ambao sio taasisi kubwa, kutoa sio utajiri bali ni moyo, msichoke kusaidia jamii kwani kwa sasa wanafunzi wanaojiunga kidato cha kwanza wanaongezeka kwa kasi kila mwaka.  Ningependa siku nyingine tuitane kwenye jambo kubwa zaidi.” Alisema Mfune

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Bi Anyubatile Seme amelishukuru shirika hilo kwa kuacha alama hasa kwenye akili za wanafunzi kwani kitendo cha kutoa madawati 52 ni kikubwa sana na ni chachu kwa mashirika menginge kuiga mfano  huo mzuri kwani walichokifanya PESCODE VICOBA kitasaidia kupunguza uhaba wa madawati.

Akisoma Risala kwa niaba ya wanachama wa vikundi vya VICOBA, Bwana Elieza Kagusi alisema kwamba PESCODE VICOBA ilianza kufanya kazi katika Wilaya ya Mbarali mwaka 2014 katika kata 13 na mpaka sasa wameanzisha na kusimamia vikoba 50 ambavyo vipo kata za Mahongole, Madibira, Ubaruku, Rujewa, Lugelele, Mapogoro, Chimala, Ihahi, Itamboleo, Utengule Usangu, Igurusi na Kongoro Mswisi.

Bwana Kagusi aliongeza kuwa shirika lao linajishughulisha na utoaji wa elimu  ya uanzishwaji wa vikundi vya kijamii vinavyojishughulisha na uwekaji wa akiba, kukopeshana na pia kutoa elimu ya usimamizi, ujasiliamali, mafunzo ya uongozi pamoja na uandaaji wa taarifa

Katika Halfa hiyo ya makabidhiano Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mhe. Reuben Mfune amewashukuru wananchi wote wa Mbarali wanaohamasika katika ujenzi wa miundombinu ya shule za sekondari pamoja na uchangiaji wa madawati kwani kwa sasa hali inaridhisha.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, NOVEMBA 27,2024 October 20, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 17, 2024
  • MPANGO MKAKATI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBARALI 2018_2019- 2022_2023 June 08, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELO KIASI CHA SHILINGI 1,010,267,500.00 March 13, 2021
  • Tazama

Taarifa Mpya

  • DC MBARALI UFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KATA YA ITAMBOLEO

    May 22, 2025
  • ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI WA MBARALI KUJIFUNZA BIASHARA YA HEWA YA KABONI

    May 22, 2025
  • ZIARA KAMATI YA SIASA YA MKOA WA MBEYA WILAYANI MBARALI

    May 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI

    May 16, 2025
  • Tazama

Video

MBUNGE MBARALI ATOA MILINI 120 KWA AJILI YA SARE WANAFUNZI WOTE WALIOFAURU KIDATO CHA KWANZA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Google
  • SAIRLA TANZANIA DASHBOARD

Tovuti Mashuhuri

  • RAS Mbeya Web Site
  • Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Salary Slip Portal

Ramani kwa wasafiri

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana Nasi

    Rujewa Road 3 km from main Road: Then Drive Mkurugenzi road. 1

    Sanduku la Posta: 237 Rujewa Mbeya

    Simu ya Mezani: 252957440/252957447

    Mobile: +255784 906 216

    Barua Pepe: ded@mbaralidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Copyright ©2021 GWF . All rights reserved.